MABINGWA wa ligi kuu soka
Tanzania Bara Simba Sc, kesho watashuka katika uwanja wa Qaboos Sports Complex
nchini Oman
kukwaana na timu ya Taifa ya huko iliyoshiriki michuano ya Olimpiki,
imefahamika.
Simba ipo nchini Oman kwa kambi
maalum ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu soka Tanzania Bara na michuano ya kimataifa.
Katibu Mkuu wa Simba Evodius
Mtawala ameiambia Sports Lady leo kwamba mchezo huo utakuwa ni muhimu kwa timu hiyo kwani
kocha atautumia katika harakati zake za kukisuka ipasavyo kikosi chake.
“Kama
mnavyojua tangu tumpate kocha mpya (Patrick Liewing) kikosi hajipata kukaa
pamoja hivyo huo ndio mwanzo wa kocha kuanza kukiweka sawa kikosi chake,”alisema
Mtawala aliongeza kuwa, kocha
Liewing amefurahishwa na wachezaji wote kuwa pamoja kwa sasa ambapo anaamini
kambi hiyo itakuwa na mafanikio zaidi.
Mbali na mchezo huo, Simba
inatarajiwa kucheza mechi nyingine za kirafiki na timu kama
Fanja Fc na timu ya jeshi la huko kabla ya kurejea nchini Januari 23.
Comments
Post a Comment