WAKATI uchaguzi wa viongozi
wa Chama cha Makocha wa Soka Tanzania (TAFCA) ukitarajiwa kufanyika Januari 19
kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, wagombea watano tu ndio watakaochuana kwenye nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura
amesema leo kwamba maandalizi kwa ajili ya uchaguzi huo yanakwenda vema.
Alisema alisema mkutano huo
wa uchaguzi kabla ya kufanyika kwa zoezi hilo
utatanguliwa na mkutano mkuu wa Tafca, huku akitoa wito kwa vyama vyote vya
mikoa vinatakiwa kuwasilisha majina ya viongozi waliochaguliwa katika mikoa yao kwa kamati ya uchaguzi
kabla ya Januari 17.
Wambura amewataja waliojitosa
kuwania uongozi katika chama hicho ni pamoja na Oscar Korosso na Lister (Uenyekiti),
Michael Bundala (makamu Mwenyekiti),
Wilfred Kidau na Lugora wanaowania nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.
Aidha, Wambura aliongeza kuwa
kutokana na kutokuwepo kwa wadau walioomba kuwania nafasi za Uhazini na Katibu
Mkuu, nafasi hizo zitajazwa katika mkutano utakaoitishwa baadaye.
Comments
Post a Comment