FUNGU la pili la wachezaji wa
klabu ya Simba, linatarajiwa kuondoka jijini leo jioni kwenda Oman kuungana na
wenzao walioweka kambi kwa ajili ya kujiwinda na Ligi Kuu Bara na michuano ya
kimataifa.
Awali, fungu la kwanza
likiongozwa na Kocha Mkuu Patrick Liewing na Meneja wa timu, Moses Basena liliondoka
juzi kwenda huko kwa ajili ya kambi hiyo maalum ya maandalizi.
Kocha Msaidizi, Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’ ambaye alibaki na kundi la pili kwa ajili ya mchezo wa nusu
fainali ya Kombe la Mapinduzi linaloendelea visiwani Zanzibar, kabla ya
kutolewa na Azam Fc juzi usiku, ndiye atakayeongoza msafara huo.
Julio, aliwataja wachezaji
watakaoondoka leo kuwa ni pamoja na William Mweta, Miraji Adam, Paul Ngalema, Hassan
Isihaka, Komabil Keita, Jonas Mkude, Ramadhan Singano ‘Messi’, Abdallah Seseme
na Said Demla.
Kundi jingine la wachezaji wa
Simba, litahusisha waliopo timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ ambayo ipo nchini
Ethiopia, ambao wataungana na wenzao kesho.
Simba ambayo itaiwakilisha
Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika, itaanza kwa kucheza na
Recreativo do Libolo ya Angola kati ya Februari 17 na 19 jijini Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment