WAKATI
klabu za Esperance na Etoile du Sahel za Tunisi zikimkana
mshambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi, imebainika kwamba nyota huyo yupo nchini
kwao Uganda.
Hivi
karibuni baadhi ya vyombo vya habari nchini vilimkariri Mwenyekiti wa Simba
Alhaj Ismail Aden Rage akisema kwamba nyota huyo ameshindwa kujiunga na wenzake
kutokana na kuwa nchini Tunisia akifanya majaribio katika klabu ya Esperance.
Uchunguzi
uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umethibitisha kwamba nyota huyo ambaye
amekuwa akiiumiza sana kichwa klabu yake ya Simba hayupo nchini humo kama
ilivyoripotiwa.
Akizungumza
na Tanzania Daima Jumapili, Rage alizikana taarifa za Okwi kujaribiwa Esperance
na kudai kwamba anajaribiwa Etoile Du Sahel.
“Okwi hayupo
Esperance bali ni Etoile Du Sahel…anaendelea na majaribio yake na kama kutakuwa
na taarifa zozote mtaarifiwa,”alisema
Hata hivyo,
mwandishi wa habari hizi aliwasiliana na Mwenyekiti wa Etoille Ridha Charfeddine
ambaye alikana kuwepo kwa mchezaji huyo anayefanya majiribio katika timu yao.
“Hatuna
mchezaji anayeitwa Okwi kwenye timu yetu…pia hatuna mchezaji yoyote kutoka
Uganda ambaye tunamfanyia majaribio,”alisema
Tanzania
Daima Jumapili lilipomtafuta tena Rage ili kujua ukweli wa taarifa hizo
halikufanikiwa kumpata baada ya simu zake kutokuwa hewani.
Okwi ambaye
mwioshoni mwa mwaka uliopita alisaini mkataba mpya wa kuitumikia Simba, amekuwa
na tabia ya kuumiza vichwa vya viongozi wa timu hiyo pindi anapoenda likizo
kwao kwa kushindwa kurejea nchini kwa wakati anaotakiwa.
Rage pamoja
na mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hanspoppe walimfuata Okwi
kwa Uganda alipokuwa akiitumikia timu yake ya Taifa ‘The Cranes’ katika
michuano ya Chalenji na kumsainisha mkataba mpya.
Hali hiyo
imepelekea uongozi kumfuta katika safari ya Oman ambapo Simba ipo huko kwa
kambi maalum ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom pamoja na
michuano ya kimataifa ambapo itashiriki klabu bingwa ya Afrika itakapoanza
kampeni kwa kucheza na Recreativo do
Libolo ya Angola kati ya Februari 17 na
19 jijini Dar es Salaam.
Hii ni mara
nyingine tena ya kuyibuka kwa utata wa mchezaji huyo kujaribiwa nje baada ya
mwezi Julai mwaka jana kudaiwa kufanya majaribio katika klabu ya Redbull
Salzburg ya Austria huku viongozi wakitoa taarifa za kujichanganya.
Viongozi hao
walidai Okwi kufuzu majaribio hayo na hivyo wangemuuza kwa Euro 600,000 (sawa na Sh. bilioni 1.1), kabla ya
baadaye nyota huyo kukana kufanya majaribio katika klabu hiyo.
Okwi aliweka
wazi kwamba hakuwahi kufanya majaribio hata siku moja nchini Austria kwani
tangu alipotua huko alikuwa mgonjwa hivyo kutokana na kuugua, uongozi ulimtaka arejee
nyumbani na hadi atakapoitwa tena.
Katika hatua
nyingine, Simba inatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza keshokutwa dhidi
ya Olimpiki ya Oman, kabla ya Januari 18
kuikabili Suwqi na baadaye kupiamana
ubavu na Fanja FC.
Comments
Post a Comment