UHAI CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI DESEMBA 7


Michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu za U20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom inatarajia kuanza Desemba 7 mwaka huu na kumalizika Desemba 22 mwaka huu. 
Wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ni wale tu ambao usajili wao umefanyika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kupata leseni. Hakutakuwa na usajili mwingine wowote mbali na ule uliofanyika sambamba na wa Ligi Kuu. 
Taratibu zote za michuano hiyo zitafahamishwa kwa klabu husika ikiwemo ratiba ya michuano hiyo.

Comments