HATIMAYE mshambulaiji wa kimataifa wa
Simba, Mganda Emmanuel Okwi ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea
kuichezea timu hiyo.
Awali kulikuwa na hatihati ya Simba kumkosa
mchezaji huyo ambaye alitaka dola 40,000 ili aweze kusaini mkataba mpya, kabla
mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zakaria Hans Poppe kuokoa jahazi.
Zoezi la kusaini mkataba huo lilifanyika
jana usiku nchini Uganda ambapo zoezi hilo limesimamiwa na mwenyekiti wa Simba
Alhaj Ismail Ade Rage pamoja Hans Poppe.
Comments
Post a Comment