Safari kubwa ya mwishoni mwa mwaka ambayo inawakutanisha
vijana kutoka sehemu mbalimbali ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania kwa ajili
ya kwenda kusheherekea kwa pamoja sherehe za mwaka mpya inatarajiwa kufanyika
tena mwaka huu kwa jumla ya siku nne mfululizo visiwani Zanzibar kuanzia
Desemba 31, 2012 mpaka Januari 3, 2013 ikiwa na lengo la kuwaleta vijana pamoja
na kutangaza utalii wa ndani hapa nchini kwa.
Safari hiyo ambayo imekuwa na mafanikio tangu kuanzishwa
kwake mwaka 2010/2011 na vijana watatu wa Kitanzania waliokuwa wanachama wa
Taasisi ya Kimataifa ya Vijana walio katika Elimu ya juu inatarajiwa
kushirikisha vijana takribani 100 kutoka pande zote za Dunia na Tanzania kwa ujumla katika kusheherekea kwa
pamoja visiwani Zanzibar .
“Zanzibar Reloaded tumekuwa tukifanya hivi kila mwaka kwa
kutoa nafasi kwa vijana wa Kitanzania na nje ya nchi kuweza kujumuika pamoja na
kusheherekea kwa pamoja katika kaudhimisha ujuo wa mwaka mpya ikiwa na pamoja
na kutafakari changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana na nini mipango ya
kila kijana katika kukabiliana na changamoto hizo” Alisema Ndg. Gwamaka
Mwibuka, Mkuu wa Maandalizi wa Zanzibar Reloaded.
Safari hii haibagui mtu yeyote kutoka upande wowote ule wa
Dunia kuweza kujumuika pamoja na vijana wenzake kushiriki katika sherehe hizi,
kwani nia ni kutengeneza Muunganiko mmoja wa vijana toka pande zote za Dunia.
“Hii si safari ya baadhi ya kikundi cha vijana bali ni
safari ya kila kijana ambae anapenda kwenda kufurahia sherehe za mwaka mpya
katika visiwa vya marashi ya karafuu huku akitembelea sehemu muhimu za utalii
visiwani humo, ukiangalia viwango vilivyowekwa vinaendana na huduma
itakayotolewa kwa siku zote nne tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho”.
Aliongeza Gwamaka
Akitaja viwango vya mchango wa Safari hiyo kwa mtu mmoja ni
Shilingi 150,000/= kwa Mtanzania na Dola 160 kwa mgeni anae nje ya nchi na
kufafanua kwamba pesa hizo zitatumika kwa Usafiri wa Boti Dar-Zanz kwenda na
kurudi, Malazi siku zote nne, Chai, usafiri wa kutembea sehemu mbalimbali,
Parties na kiingilio cha Clubs kwa watakaopenda kwenda lakini akafafanua zaidi
na kusema kwamba mshiriki atajihudumia chakula cha mchana na usiku kwa siku
zote hii ni kutoa fursa ya mtu kula kile anachokipenda ikiwa na kunywa
anachokipenda.
“Mwaka huu tumejipanga kuacha kumbukumbu ya daima ndani ya
vichwa vya watakaoshiriki, tutakwenda kutembelea Prison Island, Dolphin Tour
nayo itakuwepo, Tutapata muda wa kutembelea Stone Town na kufanya Shopping,
Kuogelea na kucheza kwa pamoja katika fukwe za bahari visiwani humo”.
Alimalizia Gwamaka.
Unaweza kufanya Booking yako sasa kupitia website:
http://zanzibarreloaded.wix.com/2013, Au ukurasa wa Facebook:
https://www.facebook.com/ZanzibarReloaded kwa picha na taarifa zaidi.
Zanzibar Reloaded ilianza mwaka 2009/2010 ambapo Vijana
watatu wa Kitanzania ambao waliungana pamoja na kutafuta njia nzuri ya kumaliza
mwaka mpya kwa vijana wote wa Tanzania
na nje ya Tanzania
kwa lengo ya kubadilishina mawazo pamoja.
Zaznibar Reloaded ni tukio la kila mwishoni mwa mwaka ambalo
hufanyika katika visiwa vya Zanzibar ,
tukio ambalo lina lengo la Kusheherekea na kuwaleta vijana kutoka sehemu
mbalimbali za Dunia kwa ajili ya Kufurahi pamoja na kutengeneza muunganiko
imara hii ikiwa pamoja na kujionea maajabu yaliyopo visiwani ambayo
yataimarisha na kuhamasisha utalii wa ndani.
Comments
Post a Comment