'MZIMU WA BONGO DANSI UNAOENDELEA KUTESA UGHAIBUNI'


Mwaka 2012 ndio unakwisha na Mzimu wa "Bongo Dansi " unaendelea kusumbua vichwa Ughaibuni !
 Hakuna mashaka yeyote unapoutaja muziki wa Tanzania katika Nyanja za kimataifa.
Jina la Ngoma Africa band maarufu pia kama  “FFU Ughabuni” inayoongozwa na Mwanamuziki Kamanda Ras Makunja wa FFU mwenye kukaanga mbuyu na wa Kuwachia wenye meno kutafuna.
Kamanda Ras Makunja na kikosi chake hicho Ngoma Africa band yenye maskani yake Nchini  Ujerumani,Ughaibuni ndio wanao zidi kuwatia wazimu washabiki wa muziki Barani ulaya kwa kuitangaza miziki ya Tanzania na kiafrika kwa kasi kubwa barani ulaya. 
Bendi  hiyo maarufu  iliyoanzishwa mwaka 1993 na kiongozi wake Ebrahim Makunja Almaarufu Kamanda Ras  Makunja,imeweza kufanikiwa kuwapo katika medani ya muziki Na kuweza kukonga nyoyo za washabiki tangu ilivyoanzishwa,pamoja na mafanikio hayo ambayo sio kitu rahisi kuyafikia kwa bendi za kiafrika barani ulaya,lakini kamanda Ras Makunja na mzimu wake huo Ngoma Africa band inaonekana kuwa ni hekalu la ajabu!
Watafiti na taasisi mbali mbali za kimataifa za mambo ya itifaki katika medani ya muziki zimeelezea bendi hiyo kuwa na washabiki au wapenzi wapatao milioni hamsini (Milioni 50) kila kona duniani kote, na kuifananisha bendi hiyo kuwa sawa na na muzimu mkubwa wenye mvuto na mtandao   wa mamilioni ya watu!
Watafiti wanashangazwa sana sana kuona kuwa bendi hiyo maarufu ya kiafrika barani ulaya imekuwa na mvuto mkubwa kwa washabiki,hadi sasa watafiti hawajagundua siri inayoifanya bendi hiyo kuwavuta washabiki kwa wingi!
Tunapozungumzia  umaarufu na ustadi wa Ngoma Africa Band ni sawa na kuzungumzia Moto Mkali wa  nyikani Usiozimika ! na washabiki wake wapo tayari katika kila hali kuutetea mzimu wao „Ngoma Africa Band“ ukipenda FFU.
 Ngoma Africa band na Ushindi wa International Diaspora Award 2012, Juhudi za harakati za bendi ya Ngoma Africa zimevuna matunda makubwa licha ya kuwanasa mamilioni
Ya washabiki wa kimataifa bendi hiyo imeweza kuchagulia kuwa bendi bendi bora katika maonyesho mengi ya
Kimataifa yakiwemo maonyesho ya “Expo 2000 Hannover” Germany na “Pacific World Music Festival 2000,Honolulu,Hawai. 
Mwaka huu 2012 Kiongozi wa bendi hiyo Kamanda Ras Makunja alitunikiwa tuzo ya kimataifa ya (IDA) International
Diaspora Award,kwa niaba ya bendi yake mjini Tubingen,Germany.
Ngoma Africa band inatajwa kuwa ndio bendi ya kwanza ya kigeni barani ulaya kupewa tuzo hiyo ya kimataifa ,kutokana
Juhudi za bendi hiyo za kuutangaza muziki na utamaduni kiafrika.
Kutokana na taarifa za tahasisi ya Africa-activ Organizatation yenye makao yake Reutlingen, Ujerumani zinailezea bendi
Hiyo kuwa ni urimbo mkali unaowanasa mamilioni ya washabiki mara moja na mamilioni ya  washabiki wapo taabani
Kwa mapenzi na mzimu huo wa muziki Ngoma Africa band. Sili iliyiomo ndani ya bendi hakuna anayejua !! Labda
Mwenyewe Ras Makunja. 
Wataalamu  mbali mbali wa sosholojia na  sekolojia ya maswala ya kijamii wanaizungumzia bendi ya Ngoma Africa
Kuwa ni jinamizi lenye nguvu kubwa za ajabu,jinamizi ambalo limetumia muziki wake kuwateka washabiki barani
Ulaya ! haijulikani nini siri ya mvuto huo ! Jinamizi hili la “Bongo Dansi” ! pia limewapa wakati mgumu bendi nyingi
Sana zinazo shea majukwaa katika maonyesho ya kimataifa.
 Ngoma Africa band ukipenda waiite FFU ni bendi inayomilikiwa na washabiki na wapenzi wa bendi hiyo ambao
Wapo kila kona duniani,na mafanikio haya ni mafanikio ya kujivunia watanzania. 
Ngoma Africa Band imeweza kuutawanya muziki wake katika vituo mbali mbali vya redio vya kitaifa na kimataifa,
Zikiwemo redio za afrika mashariki na ughaibuni,pia nyimbo hizo zinasikika katika mtandao au tuvoti ya bendi hiyo

Comments