KUZIONA YANGA V TUSKER KESHOKUTWA BUKU TANO TU

Mratibu wa mechi ya kimataifa ya kirafiki kati ya Yanga na Tusker ya Kenya, George Wakuganda (Kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na mchezo huo utakaopigwa keshokutwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kushoro ni ofisa habari wa Yanga, Baraka Kizuguto.
Tayari Tusker imeshawasili jijini Dar es Salaam ambapo viingilio ni sh 15,000 kwa VIP A, sh 10,000 kwa VIP B, sh 7,000 kwa watakaokaa VIP C na sh 5000 kwa wataokaa viti vya orenji na blue.

Comments