Kocha Mkuu wa timu ya Zambia (Chipolopolo) ambayo ni
mabingwa wa Afrika, Herve Renard ametaja kikosi cha wachezaji 24 kitakachoikabili
Taifa Stars kwenye mechi ya kirafiki itakayochezwa Desemba 22 mwaka huu jijini
Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Zambia (FAZ),
wachezaji hao ni Chintu Kampamba, Chisamba Lungu, Christopher Katongo, Danny
Munyau, Davy Kaumbwa, Derrick Mwansa, Evans Kangwa, Felix Katongo na Francis
Kasonde.
Wengine ni Given Singuluma, Hichani Himonde, Isaac Chansa,
James Chamanga, Jimmy Chisenga, Jonas Sakuwaha, Joshua Titima, Kalililo
Kakonje, Moses Phiri, Mukuka Mulenga, Rainford Kalaba, Rodrick Kabwe, Salulani
Phiri, Shadrack Malambo na Stoppila Sunzu.
Comments
Post a Comment