Coastal Union
ya Tanga imeendelea kufanya vizuri kwenye michuano ya kuwania Kombe la Uhai
inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 wa klabu za Ligi Kuu ya
Vodacom baada ya jana (Desemba 12 mwaka huu) kuifunga Toto Africans mabao 3-1.
Mabao ya Coastal katika mechi hiyo ya kundi A
iliyochezwa Uwanja wa Chamazi yalifungwa na Mohamed Miraji dakika ya 44, Abdul
Banda (dk. ya 62) na Ramadhan Shame (dk. ya 83). Toto Africans ndiyo iliyoanza
kupata bao dakika ya 30 lililofungwa na Severin Constantine.
Coastal Union ilishinda mechi yake ya kwanza
mabao 2-1 dhidi ya Tanzania
Prisons katika michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa
kupitia maji Uhai.
Nayo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1
dhidi ya African Lyon katika mechi ya kundi B iliyochezwa leo asubuhi (Desemba
12 mwaka huu) Uwanja wa Karume. Miraji Athuman na Ramadhan Mzee ndiyo
walioifungia Simba dakika ya 15 na 47 wakati la African Lyon lilifungwa dakika
ya 57 na Mbela Kashakala.
Polisi Morogoro iliifunga Azam bao 1-0 kwenye
Uwanja wa Karume wakati katika Uwanja wa Azam, JKT Ruvu iliifunga Tanzania
Prisons bao 1-0 lililofungwa dakika ya 16 na Jacob Mambia. Yanga na Ruvu
Shooting zilitoka suluhu kwenye Uwanja wa Chamazi.
Katika mechi iliyochezwa leo asubuhi (Desemba
13 mwaka huu) Uwanja wa Karume, Oljoro JKT imeizamisha Kagera Sugar mabao 3-0.
Mabao hayo yamefungwa na Hamis Saleh dakika ya 49 huku Shamir Mohamed
akipachika mawili dakika ya 52 na 55.
Michuano hiyo itaendelea kesho (Desemba 14
mwaka huu) kwa michezo kati ya Mtibwa Sugar vs Toto Africans (asubuhi- Karume),
Coastal Union vs JKT Ruvu (mchana- Karume), Oljoro JKT vs Yanga (asubuhi-
Chamazi), Ruvu Shooting vs Kagera Sugar (mchana- Chamazi), Mgambo Shooting vs
Simba (asubuhi- Chamazi) na African Lyon vs Azam (jioni- Chamazi).
Comments
Post a Comment