Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) litatuma ofisa
wake nchini mwezi ujao kwa ajili ya kufanya ukaguzi kwenye klabu za Ligi Kuu ya
Tanzania
kabla ya kutoa leseni kwa zile ambazo zitakuwa zimekidhi vigezo vilivyowekwa. Ili klabu ishiriki mashindano ya CAF ni lazima iwe na
leseni hiyo.
Kwa mujibu wa CAF, ofisa huyo atakuwa nchini kuanzia Januari
7 mwakani ambapo atafanya ukaguzi huo hadi Januari 14 mwakani. Mbali ya ukaguzi
katika klabu, pia ofisa huyo atakagua viwanja vitakavyotumika katika mashindano
yake na hoteli ambazo timu kutoka nje zitakuwa zinafikia kabla ya mechi.
Baadhi ya masharti kabla ya klabu kupewa leseni ya CAF ni
pamoja na kuwa na ofisi (physical address), uwanja wake wa mazoezi, programu ya
maendeleo kwa vijana, sekretarieti ya kuajiriwa, hesabu za fedha zilizokaguliwa
(audited accounts) na benchi la ufundi linaloundwa na watu wenye sifa
zinazostahili.
Comments
Post a Comment