MABINGWA wa kombe la Kagame,
Yanga wanatarajiwa kuzileta nchini timu kubwa mbili kutoka moja ya nchi za
Afrika ambazo zitacheza mechi ya kirafiki na timu yao na timu nyingine hapa nchini.
Mwenyekiti wa Kamati ya
Mashindano ya Yanga, Abdallah Binkleb (pichani) ameiambia Sports Lady hivi karibuni kwamba, wameamua
kuzialika timu hizo ili kuja kuipa makali timu yao ambayo itakuwa katika maandalizi ya
mzunguko wa pili wa ligi kuu bara na michuano ya Kagame.
Alisema tayari wameshatuma
maombi kwa timu kadhaa ambapo bado hazijatoa majibu kama
zimekubali mwaliko huo au la, hivyo wataziweka wazi pindi zitakapothibitisha.
Binkleb aliongeza kuwa kwa
sasa hawawezi kuzitangaza timu nwalizozialika wakihofia kuchanganya mambo
ikiwemo kuingiliana na mawakala katika suala hilo .
Tayari, uongozi wa Yanga chini
ya Mwenyekiti wake Yussuf Manji umetangaza kuipeleka timu hiyo nchini Uturuki
mwezi Desemba kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa
ligi kuu na michuano ya Kagame.
Katika hatua nyingine,
Binkleb alisema hawana mpango wa kuacha mchezaji katika timu hiyo,zaidi
watakachokifanya ni kuwapeleka kwa mkopo katika baadhi ya timu wachezaji ambao
wanaona wameshuka viwango.
“Suala la kujua nani
atatolewa kwa mkopo lipo kwa kocha mkuu na sisi kama
viongozi ndio tutaangalia ni wapi ambapo atahitajika kupelekwa,”alisema Binkleb
Comments
Post a Comment