Samatta
Ulimwengu
SHIRIKISHO la soka Tanzania
(TFF) limeandika barua kwa Cgama cha Soka cha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ili
kuwasaidia kuruhusiwa kwa wachezaji wa Tanzania wanaocheza katika klabu ya TP
Mazembe ya huko, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
Hatua hiyo inafuatia uongozi
wa TP Mazembe chini ya Rais wake Moise Katumbi kugoma kuwaruhusu wachezaji hao
kujiunga na timu ya Taifa ya Bara ‘Kilimanjaro Stars’ inayoshiriki michuano ya
Chalenji inayoendelea nchini Uganda.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema jana kwamba wameamua
kupitia kwa Chama hicho baada ya TP Mazembe kutowaruhusu nyota hao kwa madai
kuwa timu inakabiliwa na michezo kadhaa.
Alisema kwa sasa timu hiyo
haina mashindano yoyote, hivyo ingekuwa vema kuwaruhusu wachezaji hao ili
waweze kuisaidia Kili Stars katika hatua ya roibo fainali iwapo itafuzu.
“Rais wa TFF, (Tenga)
alishaongea na uongozi wa TP Mazembe, kabla ya kuongea na rais wa Fay a
Congo walipokutana katika mkutana wa
viongozi wa CECAFA, lakini tumeona tutume na barua ili kusisitizia sula
hilo,”alisema Osiah.
Aidha, Osiah alisema anaamini
suala hilo litashughuliwa ili wachezaji hao waweze kuruhusiwa kwa sasa
kuituymikia timu ya Taifa na pindi Tp Mazembe itakapowahitaji wataenda
kuitumikia,”alisema Osiah.
Comments
Post a Comment