SUPER D APANIA KUPELEKA VIJANA WAKE OLIMPIKI 2016



 Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akiwa katika picha ya pamoja na vijana waliojitokeza katika mazoezi ya ngumi ufukwe wa GYKHANA Dar es salaam jana Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com 

KLABU ya ngumi ya Ashanti Ilala imeota kuwa moja ya klabu itakayotoa wawakilishi katika michezo ya Olimpiki itakayofanyika mwaka 2016  nchini Brazil.
Klabu hiyo ambayo kwa sasa inaundwa na chipkizi 18 pamoja na mabondia wakongwe imepania kufanya hivyo huku ikijitapa kuwa itaanza kufanya maajabu kupitia mashindano ya taifa ya mchezo huo yatakayofanyika Januari mwakani.

Akizungumza na gaazeti hili Dar es Salaam jana, Kocha wa ngumi wa klabu ya Ashanti  pamoja na timu ya Mkoa wa Ilala Kimichezo Rajabu Mhamila 'Super D' alisema kwa sasa klabu yake imejikita katika maandalizi kabambe kuhakikisha inaingiza mabondia wengi katika timu ya taifa ambao baadaye wataingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi za kufuzu kucheza Olimpiki.
 
Alisema tayari jumla ya vijana 18 wanajifua katika Ufukwe wa Gymkhana Dar es Salaam kwa ajili ya mapambano mbalimbali ikiwemo ya ubingwa wa taifa ambayo yanaandaliwa na Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT).
 
Alisema vijana wengi waliopo kwenye klabu hiyo ni wenye umri chini ya miaka 12 na chini ya miaka 20 ambapo amewataja kuwa umri huo ni mzuri kwani kijana atakuwa mwepesi wa kuelewa kile ambacho atakuwa anafundishwa na makocha wake

Super D ambaye anafundisha kwa kutumia mbinu mbalimbali zikiwemo kwa njia ya DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani

Super D ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi


Comments