SKYLIGHT BAND YAZIDI KUWAKAMATA MASHABIKI KATIKA KIOTA CHA THAI VILLAGE MASAKI-JIJINI DAR


Vijana wa SKYLIGHT BAND wakiongozwa na Sam katika kuhakikisha mashabiki wa SKYLIGHT BAND wanapata flava za ukweli zikiwemo Kwaito, Ragga, Reggae, Dance Hall, Nigerian Flava, Sebene na zingine kibao. Kushoto ni Joniko Flower na kulia ni SONY MASAMBA. Wanapiga show ya kufa mtu kila Ijumaa katika ukumbi wa Thai Village Masaki jijini Dar es Salaam.

Mary Lukas sambamba na Joniko Flower wakitoa burudani.

SONY MASAMBA akishusha mistari.

Msanii wa SKYLIGHT BAND Aneth Kushaba AK 47 akionyesha umahiri wake wa kucheza kwa mashabiki.

Aneth Kushaba AK 47 akiwapa raha mashabiki wake (hawapo pichani).
CEO wa Ndege Insurance Dkt. Sebastian Ndege sambamba na mashabiki wa SKYLIGHT BAND wakiserebuka.
Warembo wakisakata rhumba kwa raha zao.
Pichani Juu na Chini ni Umati wa mashabiki waliojitokeza katika Kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar es Salaam kushangweka na SKYLIGHT BAND mwishoni wa wiki, ni Kila Ijumaa wako hapo.
Namba ya Mashabiki ikizidi kuongezeka kama inavyoonekana pichani, palikuwa hapatoshi. Usikose Ijumaa hii.
Couples waliong'ara siku hiyo ni hawa hapa.
Blogger King Kif (kushoto), Mdau John Mwansasu na wadau wengi wakipozi kwa picha.
Mashabiki wapya All the way from Nairobi wakipata ukodaki na Msanii wa SKYLIGHT BAND Aneth Kushaba AK47.
Watasha nao ndani nyumba chezea SKYLIGHT BAND wewe......!!!
Bongo Movie Star Steve Nyerere, Mboni Masimba a.k.a Kim Kardashian wa Bongo na Mdau John Mwansasu wakipata Ukodaki.
Mdau akipozi na warembo.
Warembo katika pozi ndani ya SKYLIGHT BAND.
Adrian Hillary Stepp, Blogger Cathbert Angelo wa Kajunason Blog na Blogger King Kif.
The Don Shaban Mazua (kushoto) akila ukodaki na wadau.

Comments