Timu
ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imetua salama mjini Congo Brazaville tayari kwa mchezo wa marudiano na wenyeji utakaopigwa kesho ugenini.
Timu hizo zinakwaana katika mchezo wa kuwania
kufuzu fainali za Afrika kwa vijana wa umri huo ambapo Serengeti itashuka dimbani ikiwa mbele kwa bao 1-0 ililolipata katika mchezo
wa awali uliopigwa wiki iliyopita katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kwa hali hiyo Stars inahitaji
kushinda ama sare yoyote ili kuweza kufuzu fainali hizo hizo kwa mara ya
kwanza.
Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah ameiambia Sports Lady kwamba anaamini
timu hiyo itatimiza wajibu wake ipoasavyo na kushinda mchezo huo, hivyo kukata
tiketi ya kucheza fainali hizo.
Alisema, kikosi hicho
kiliwasili salama nchini humo na kupata sehemu nzuri ya malazi pamoja na uwanja
wa kufanyia mazoezi kujiandaa na mchezo huo huku wachezaji wakiahidi ushindi.
Comments
Post a Comment