Shirikisho la soka Tanzania
(TFF) limewataka Watanzania kutoibeza timu hiyo, badala yake kuiunga mkono.
Stars ipo nchini humo
ikishiriki michuano ya Chalenji inayoendelea nchini humo, juzi ilianza kwa
ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Sudan.
Rais wa TFF, Leodger Tenga
alisema jana kwamba baadhi ya watu wamekuwa wakiibeza timu hiyo na hasa kudai
wachezaji wake wamezeeka kitu ambacho si
cha kweli kwani wengi wao wana miaka 28 kushuka chini.
Alisema ni vizuri kuwatia
moyo wachezaji wa timu hiyo ili waweze kuwa na ari kubwa, hivyo kufanya vizuri
zaidi katika michuano hiyo mikubwa.
Akizungumzia mchezo wa leo,
kocha mkuu wa Stars, Kim Poulsen alisema kwamba vijana wake wapo kamili kwa
mchezo huo na ili waweze kuifunga Burundi ni lazima wacheze kwa kasi na pasi za haraka.
“Lazima tucheze kwa kasi kubwa sana tena
kushinda ule mchezo na Sudan Jumapili kwani Burundi ni timu nzuri lakini
tutawabana.”
Comments
Post a Comment