KOCHA mkuu wa Simba Mserbia
Milovan Cirkovic ameutaka uongozi wa timu kuhakikisha inambakiza kundini kiungo
wake aliyesimamishwa, Haruna Moshi ‘Boban’.
Boban pamoja na beki wa timu
hiyo Juma Nyoso ambao walisimamishwa hivi karibuni kutokana na utovu wa nidhamu.
Kiongozi mmoja wa Simba
aliliambia gazeti hili jana kwa Milovan alitoa wosia huo muda mfupi kabla ya
kutimkia kwao Serbia kwa mapumziko na
kusema kwamba Boban ni mchezaji mzuri hivyo Simba kama itamtosa itakuwa
imepoteza lulu.
Alisema Milovan hakuna
mchezaji kama Boban katika ukanda wa Afrika Mashariki na hilo alilibaini
kupitia michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Kombe la
Kagame iliyofanyika nchini mwezi Agosti na Yanga kutwaa ubingwa .
“Kocha alituambia hata kama
tutaamua kuachana naye lakini tusimuache Boban kwani ni mchezaji mzuri na
kasoro alizonazo ni za kibinadamu tu…kikubwa ni uongozi kutochoka kwa kumjenga
kisaikolojia tu,”alisema kiongozi huyo.
Tayari uongozi wa Simba
umeshawapa barua za kuwataka kujieleza wachezaji hao na ndipo watatoa uamuzi
dhidi yao.
Hata hivyo kuna taarifa za
Nyoso kupelekwa kwa mkopo Coastal Union ya Tanga huku Boban akitarajiwa
kurejeshwa kundini si tu kwa ajili ya uwezo alionao bali kukikingiwa kifua na
baadhi ya watu wenye nguvu ndani ya klabu hiyo.
Uongozi wa Simba ambao kwa
sasa upo katika shinikizo la kutakiwa kujiuzulu na wanachama kutokana na
mwenendo mbaya wa timu kwenye mzunguko wa kwanza uliomalizika kwa kushika
nafasi ya tatu nyuma ya Azam Fc na Yanga inayoongoza, utakutanana wakati wowote kujadili suala
hilo.
Comments
Post a Comment