Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Juma Simba akitangaza majina ya wadau waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika chama hicho.
HATIMAYE wagombea 23 wamepitishwa kuwania uongozi katika
Uchaguzi wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), unaotarajiwa kufanyika
Desemba 12, mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya DRFA, Juma Simba, a majina hayo yamepitishwa baada ya kufanyika usaili pamoja na kujadili pingamizi
na rufaa zilizowasilishwa.
Alisema awali wagombea 36
walijitokeza na kuomba nafasi mbalimbali, kabla ya wengine kuenguliwa ama
kujitoa katika kinyang’anyiro kwa sababu mbalimbali.
Aliwataja waliopitishwa
kuwania nafasi ya uenyekiti ni pamoja na Ayoub Nyenzi, Evans Aveva, Brown Ernest na
Almasi Kasongo, huku nafasi ya Makamu Mwenyekiti itawaniwa na Meba Ramadhan,
Salum Mwaking'inda, Gungurungwa Tambaza na Ally Mayai.
Kwa upande wa nafasi ya
Katibu watakaochuana ni pamoja na Msanifu Kondo na Khamis Ambari, huku
waliopitishwa kuwania nafasi ya mjumbe
wa mkutano mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania ni Shafii Dauda, Muhsin
Balhabouh na Shufaa Jumanne.
“Wanaowania ujumbe wa kamati
ya utendaji ni Shaban Kupasya, Siza Chenja, Sunday Mwanahewa, Hamis Kisiwa, Franck
Mchaki na Baraka Mapande wakati watakaowania ujumbe kuwakilisha klabu ni Benny
Kisaka, Juma Pinto, Frank Mchaki na Philemon Ntahilaja”, alisema
Aidha, Simba aliwataja wajumbe
ambao wamechujwa ni Salum Mkemi na Juma Jabir (Uenyekiti), Issac Mazwile
(Makamu Mwenyekiti), Said Tully na Kassim Mustaffa (Katibu Mkuu), Isaack
Mazwile (Mjumbe Mkutano Mkuu TFF) na Chano Karaha (Mjumbe Kamati ya Utendaji).
Comments
Post a Comment