ALBUM YA INJILI ‘BWANA NI YESU’ IPO MTAANI

Mwimbaji chipukizi wa Nyimbo za Injili, George Haule, amipakua Albam yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la Mwamba ni Yesu na sasa ipo mtaani.

Akizungumza na Father Kidevu Blog, mtumishi huyo wa Mungu amesema albam yake ina nyimbo 8 lakini Mwamba ni Yesu ndio uliyobeba jina la albam yake hiyo ya kwanza.

Haule amewaomba watanzania na wapenzi wa nyimbo za injili nchini kumuunga mkono katika harakati zake hizo za kumuimbia Mungu.

Amezitaja nyimbo zilizomo katika labam yake hiyo kuwa ni Mwamba ni Yesu uliyobena jina la albam, Watakiri Mungu Mkubwa, Gusa Maisha Yangu, Nimeona Wala sijasimuliwa, Nadunda Mugati Mwa Yesu, Longa na Yesy, Tunapendeza na Safari na Yesu.

Haule amesema Albam hiyo ni kazi nzuri iliyofanywa na Waandaaji watatu wa muziki wa Injili, Edwad/Laulence Nguno na Muba Tach.

Amesema albam yake hiyo inasambazwa na Kampuni ya Usambazaji ya Umoja Audio Visual EA Limited au GMC kwa Mamu, na yeyote anaetaka kazi hiyo afike kwa wasambazaji hao.

Haule anatoa shukrani zake za wachungaji, viongozi na wa umini wote wa BCIC, Temeke kwa maombi yao pamoja na wote walio pokea ujumbe wa albam yake na  wakabarikiwa na wakaniombea.

Haule namalizia kwa kusema “Mungu hawezi kumuacha Mwanadamu anae mtii amina.”
 
Kwa Mawasiliano zaidi ni
+255 752644040 au +255 802405

Comments