Mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa DRFA
utakuwa kama ifuatavyo:
30/10/2012 Kamati
ya Uchaguzi DRFA kutangaza uchaguzi na nafasi
Zinazogombewa kwa mujibu wa katiba ya DRFA
31/10/2012 Kuanza
kuchukua fomu za kugombea uongozi
04/11/2012 Mwisho
wa kurudisha fomu ifikapo saa 10:00 alasiri
05-09/11/2012 Kamati ya Uchaguzi DRFA kupitia
fomu za waombaji uongozi na
kutangaza matokeo na kubandika kwenye mbao majina ya waombaji uongozi.
10-14/11/2012 Kutoa fursa ya pingamizi dhidi ya
waombaji uongozi. Pingamizi
ziwasilishwe kwa katibu wa Kamati ya Uchaguzi DRFA na
wawekaji pingamizi wazingatie Ibara ya 11 (2) ya Kanuni
za
Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
15-17/11/2012 Kujadili pingamizi, usaili na
kutangaza matokeo ya usaili na
kuwajulisha kwa maandishi.
18-20/11/2012 Kukataa rufaa dhidi ya maamuzi ya
Kamati ya Uchaguzi ya DRFA
21-25/11/2012 Rufaa kusikilizwa na Kamati ya
Uchaguzi ya TFF na kutangaza
matokeo ya rufaa (Kama hakuna rufaa, Kamati ya Uchaguzi
ya
DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi wanazogombea
na kuanza kampeni).
26/11/2012 Baada
ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya
Uchaguzi ya DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi
zao
na kuanza kwa kampeni
12/12/2012 Uchaguzi
Comments
Post a Comment