Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) ilikutana jana (Oktoba 5 mwaka huu) kupitia na kufanya uamuzi katika
masuala mbalimbali na kupanga Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ianze kutimua vumbi
Oktoba 20 mwaka huu.
Timu zimepangwa katika makundi matatu ya timu nane nane
ambapo zitacheza ligi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na ugenini. Mshindi wa kila
kundi ndiye atakayepata tiketi ya kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao
wakati timu ya mwisho kila kundi itashuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa.
Kundi A lina timu za Burkina Moro ya Morogoro, Kurugenzi
Mufindi ya Iringa, Majimaji ya Songea, Mbeya
City ya Mbeya, Mlale JKT ya Ruvuma , Mkamba Rangers ya Morogoro, Polisi Iringa na
Small Kids ya Rukwa.
Ndanda FC ya Mtwara, Ashanti United, Green Warriors, Moro
United, Polisi, Tessema, Transit Camp na Villa Squad zote za Dar es Salaam
ndizo zinazounda kundi B wakati kundi C ni Kanembwa JKT ya Kigoma, Morani ya
Manyara, Mwadui ya Shinyanga, Pamba ya Mwanza Polisi Dodoma, Polisi Mara,
Polisi Tabora na Rhino Rangers ya Tabora.
Comments
Post a Comment