WASHABIKI 65,458 WAZISHUHUDIA SIMBA, YANGA WIKIENDI


Mechi za Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara za Simba na Yanga zilizochezwa wikiendi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zimeshuhudiwa na washabiki 65,458.
 
Yanga ambayo iliibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya JKT Ruvu, Jumamosi (Septemba 22 mwaka huu) mechi yao ilishuhudiwa na washabiki 15,770 wakati ile ya Simba na Ruvu Shooting iliyochezwa jana (Septemba 23 mwaka huu) ilikuwa na washabiki 9,688. Simba ilishinda mabao 2-1.
 
Wakati mechi ya Yanga iliingiza sh. 88,251,000 ile ya Simba dhidi ya Ruvu Shooting Stars mapato yalikuwa sh. 55,454,000. Mechi ya Yanga kila timu ilipata sh. 19,846,194.92 huku ile ya Simba kila timu ilipata sh.11,350,774.58.
 
MECHI YA AZAM, MTIBWA SUGAR ZAINGIA MIL 2.5/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Mtibwa Sugar iliyochezwa juzi (Septemba 22 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi imeingiza sh. 2,509,000 ambapo kila timu imepata mgawo wa sh. 301,661.
 
Washabiki 827 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyomalizika kwa Azam kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
 

Comments