YANGA SC YAWASALISHA USAJILI WAKE TFF, TWITE NDANI


Young Africans imewasilisha jumla ya majina ya wachezaji  28 kwa shirikisho la soka nchini TFF, kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu nchini inayotazamiwa kuanza mapema septemba mosi. 

Katibu mkuu wa Young Africans Mwesigwa Selestine amesema wamepeleka majina ya wachezaji wote 28 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu, na hii ni kutokana na benchi la ufundi kuridhia kuwatumia wachezaji wote. 

Aidha katika usajili huo uliowasilishwa leo, umeambatana na usajili wa wachezaji wa timu ya vijana U-20 ambapo majina ya wachezaji mahiri wa timu ya Taifa Saimon Msuva na Frank Domayo.

Usajili  kamili kwa timu ya wakubwa ni kama ifuatavyo:

Walinda Mlango: 
Yaw Berko, Ally Mustafa 'Barthez' na Said Mohamed 

Walinzi wa pembeni:
 Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, David Luhende na Stephano Mwasika

Walinzi wa kati: 
Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondan, Mbuyu Twite, Ibrahim Job na Ladislaus Mbogo

Viungo wa ulinzi: 
Athuman Idd 'Chuji', Juma Seif Kijiko na Salum Telela

Viungo wa pembeni: 
Nizar Khalfani, Shamte Ally, Idrisa Rashid na Omega Seme

Viungo washambuliaji: 
Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo na Nurdin Bakari

Washambuliaji: 
Said Bhanaunzi, Hamis Kiiza 'Diego', Didier Kavambagu na Jeryson Tegete


 Majina hayo yanakamilisha jumla ya 28 ya wachezaji kwa timu ya wakubwa.

Kikosi cha U-20 kina jumla ya majina 22 ambao ni:

Walinda Mlango: Geofrey Nyalusi na Yusuf Abdul

Walinzi: Said Manduta, Zuberi Juma, Said Mashaka, Benson Michael, Issa Ngao, Rashid Said

Viungo: Frank Domayo, Omary Nasry, Clever Charles, Mwinyi Bakari, Mpenda Abdallah

Washambuliaji wa pembeni: Abdulahman Ally, Hussein Moshi, Abdallah Salum, Rehani Kibingu

Washambuliaji: Saimon Msuva, George Banda, Notikely Masasi, Suleiman Ussi, Kassim Jongo

NB: Frank Domayo & Saimon Msuva usajili wao umepelekwa katika usajili wa U-20 lakini wataitumikia timu ya wakubwa



http://youngafricans.co.tz

Comments