AMSHA AMSHA YA FIESTA JIJINI TANGA

Mkuu wa Vipindi wa Clouds Fm Sebastian Maganga (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo kwa watangazaji wa redio hiyo Lovenes Love na Adam Mchomvu wakati walikuwa wakiongea na wasikilizaji wa redio ndani ya Tanga katika amsha amsha ya Tamsaha la Fiesta 2012 linalotegemea kufanyika tarehe 26.8.2012 Uwanja wa Mkwakwani. Tamasha hilo litakalopambwa na msanii maarufu wa kimataifa kutoka nchini Kenya Prezzoo.
Mtangazaji wa Clouds Fm Adam Mchomvu akionyesha t-shirt ambazo zimetoka kwa ajili ya kusherekea tamasha hilo la Fiesta 2012.
Mwanadada Loveness Love akisababisha ndani ya amsha amsha ya tamasha la Fiesta linalofanyika wikend hii ndani ya Tanga.
Mkuu wa Vipindi wa Clouds Fm Sebastian Maganga akiendeleza harakati za kukamata matukio ndani ya kitaa cha Chumbageni, pale Clouds Fm ilipotembelea vijana hao wa maskani na kupata mawili mawili matatu kuhusiana na tamasha hilo.
Mazungumzo ya haopa na pale yakiendelea.
...vijana wakimsikiliza Mkuu wa Vipindi wa Clouds Fm Sebastian Maganga, pembeni yake ni Adamu Mchomvu.
Vijana walipata mzuka wa kufunguka na kuonyesha vipaji vyao.
...Mzuka ulipata na kuanza kuchana.
Mmoja ya maproducer wakali wa msanii Moraka akiongea machache mara baada ya kukutwa akiwa amekaa na vijana wenzake ndani ya maskani ya Chumbagenino.
Moja ya staili niliyokutana nayo.
Picha ya Kumbu kumbu kwa vijana wa Chumbagenino.
Mara baada ya Clouds Fm kutoka Kitaa cha Chumbageni maskani ya Chumbagenino Clouds Fm ilihamia kitaa kingine ambapo alijitokeza kijana mmoja na kuomba awe mtangazaji hapa alikuwa alimfanyia mahojiano Mwanadada Loveness Love.
Aha... Sudi Brown (kushoto) akiwa na Mchomvu.

Ukumbusho Muhiumu sana.
Aha...mambo yalinogeshwa na kuwekwa sawa. Unaweza kufuatilia kinachoendelea katika amsha amsha za tamsaha la Fiesta 2012 kupitia Kajunason Blog.

Comments