YANGA WAPELEKA 'CHEKECHEA ' ZENJI


BAADA ya awali kugoma kushiriki michuano ya kombe la Urafiki inayoendelea Visiwani Zanzibar, uongozi wa timu hiyo umeamua kupeleka kikosi chake cha pili.
Awali Yanga waligoma kushiriki michuano hiyo kwa hoja ya kuhofia majeruhi kuelekea michuano ya Kagame, juzi jioni walithibitisha ushiriki wao ambapo leo itashuka dimbani kukwaana na Jamhuri ya Pemba.
Ofisa habari wa Yanga, Louis Sendeu, alisema mapema jana mchana kuwa, kikosi kingeondoka jioni ya jana.
Hata hivyo, Sendeu alidai pia kikosi cha Yanga kingefanya mazoezi jioni ya jana kwenye Uwanja wa Kaunda akiwemo Niyonzima aliyetua akitokea kwao Rwanda.
Kauli hizo mbili tofauti za Sendeu, zilionekana kuleta utata na alipobanwa juu ya timu ipi ingekwenda Zanzibar na ipi ingebaki Kaunda, akaonekana kubabaika kabla ya kusema apigiwe simu baadaye.
Yanga, mabingwa watetezi wa michuano ya Kagame wataanza kampeni Julai 14 dhidi ya Atletico ya Burundi katika kundi C, huku Simba wakianza na URA ya Uganda.

Comments

  1. Yanga hawajiamini kiwango chao ndo maana wameshaanza sababu nyingi OOOH Yanga wamepeleka chekechea(bora wangesema Yanga wamepeleka Vibonde ili tufahamu kuwa Yanga ni vibonde.)Kwa tunaofahamu soccer wanaume wanaojiamini ni Azam na Simba ambao hatuja sikia vijisababu vya uwoga kama vya Yanga...ndo maana Simba na Azam watabakia kuwa timu bora kwa Tanzania kwa ambaye anabisha APANDE JUU YA HII..!Yanga walianza uwoga baada ya kusikia kusikia Simba wameingia kwny Kombe la Ujirani mwema ooh hatutaki kujiaribia Program yetu ya mazoezi kwa ajili ya kagame,nilipobaini Yanga wanaUWOGA ni pale walipojipima na waganda na kubahatisha matokeo jioni yake wakatangaza kujiunga na Azam pamoja na Simba...Mimi mtazamo wangu hili kombe la Ujirani mwema ni mazoezi tosha kwa ajili ya kuingia kagame,tena ndo sehemu muhimu coach anapotambua weakness ya team pamoja na players wake then unafanyia marekebisho mapungufu yake kwa ajili ya Kagame cup>>>>>au mnasemaje waungwana..?mimi ndo maana nasema Simba na Azam zitabakia kuwa club bora kwa hapa ....hata hivyo kwa africa jaribu ku_Google rank za vilabu utaona gape ya Simba na Yanga..kama sikosei Simba ni ya 20 na ushehee na Yanga B(Vibonde) ni ya 60 na ushehee sasa tofauti ni mara 3 kwa Simba kweli hiyo team...lazima utakaposikia Simba katia mguu ubaridi UKUPENYE...

    ReplyDelete

Post a Comment