Timu za AS Vita Club ya
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na URA ya Uganda zinatarajia kuwasili
nchini Julai 12 mwaka huu kushiriki michuano ya Klabu bingwa Afrika Mashariki na
Kati (Kombe la Kagame) itakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 14 mwaka huu.
AS Vita Club ambayo iko kundi
A pamoja na timu za Simba (Tanzania Bara), Ports (Djibouti) na URA itawasili saa
1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways ikipitia Nairobi.
Nayo URA itatua Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jioni ya siku hiyo kwa ndege ya Air
Uganda. AS Vita imepangiwa kufikia hoteli ya Rombo Green View wakati URA itakuwa
hoteli ya Royal Valentino.
Comments
Post a Comment