Warembo wa Redds Miss Sinza wakiwa mazoezini kwenye ukumbi wa Mawela social (Ten Star Lounge) uliopo karibu na hotel ya Vatican chini ya mwalimu wa, Mwajabu Juma ambaye anashikiria taji la Top Model . Warembo hao watapanda jukwaani Julai 13 kutafuta tiketi ya kuiwakilisha Sinza katika mashindano ya Kanda ya Kinondoni na baadaye Miss Tanzania. (Picha na Mpiga Picha wetu)
Na Mwandishi Wetu
WAKATI bendi ya African Stars (Twanga Pepeta) itapamba
shindano la kumsaka mrembo wa Redds Miss Sinza 2012 lillopangwa kufanyika
Ijumaa kwenye ukumbi wa Mawela Social (Ten Star Lounge) uliopo karibu na hotel
ya Vatican City , Kamati ya Miss Tanzania kesho itatembelea warembo hao kwa lengo la
‘kuwafunda’ tayari kupanda jukwaani.
Mratibu wa kampuni ya
Calapy Entertainment, Majuto Omary alisema jana kuwa Twanga Pepeta imeandaa
zawadi kwa mashabiki wake na wale wa urembo kwa kuwapa uhondo wa nyimbo mbili
mpya ambazo zitakuwa zinasikika kwa mara ya kwanza jukwaani.
Nyimbo hizo ni Mapambano ya Maslahi uliotungwa na Muumin
Mwinjuma, Shamba la Twanga ambao umetungwa na Greyson Semsekwa na mmoja ambao
haujapewa jina uliotungwa na Jumanne Saidi ambaye amfunga ndoa na mnenguaji wa
bendi hiyo, Asha Sharapova.
Alisema kuwa nyimbo hizo ni zawadi kwa mashabiki wa Twanga
wa Sinza na vitongoji vyake kwani bendi hiyo haijafanya shoo huko muda
mrefu.
“Tunatarajia kuwa na shoo nzuri kutoka kwa warembo na bendi
ya Twanga Pepeta ambayo mwaka huu imeshinda tuzo mbili katika tuzo za muziki Tanzania ,”
alisema.
Kuhusiana na ziara ya Kampuni ya Lino International Agency,
Majuto alisema kuwa Lundenga na wenzake watafanya mazungumzo na warembo hao
baada ya mazoezi yao
ya pamoja.
Alisema kuwa ziara hiyo ni moja ya faraja kwa warembo na
kamati ya Miss Sinza kutokana na ukweli kuwa ujio wao ni wa Baraka na hitimisho
la mashindano ya vitongoji nchini.
“Miss Sinza ndiyo inafunga pazia la mashindano ya Vitongoji
(vituo) nchini, Lundenga na wenzake wanakuja kutoa baraka zao kabla ya kuanza
pilikapilika za Redds Miss Tanzania ,”
alisema.
Shindano hilo lililodhaminiwa na Redds Premium Cold, Dodoma
Wine, Kidoti Fashion, Clouds Entertainment, sufianimafoto.blogspot.com, Lady
Pepeta na flexi P, Fredito Entertainment, Screen Masters, Brake Point na Jackz Cosmetics Kinondoni.
Comments
Post a Comment