TUZO ZA WACHEZAJI WA LIGI KUU BARA ZAJA


KAMPUNI ya Wazalendo Bright Media kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ipo kwenye mchakato wa kumpata mwanasoka bora wa mwaka 2012. 
Tuzo hizo zinajulikana kwa jina la Wazalendo Best footballer of the Year Awards, ambapo washiriki wanaoingia kwenye kinyang’anyiro hihi ni  Watanzania ambao wanacheza soka kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara. 
Kwa upande wa wageni wanaocheza Tanzania watakuwa na tuzo yao maalum ya mwanasoka bora wa kulipwa, ambayo ipo kwenye orodha ya tuzo 11 zinazowaniwa na wanasoka. 
 Tuzo hizo 11 ni pamoja na kipa, beki, kiungo, mshambuliaji, mchezaji anayechipukia, mchezaji mkongwe zaidi kwenye ligi, mchezaji bora wa kigeni, mwanasoka bora kwa wanawake, tuzo ya heshima katika maendeleo ya soka la wanawake,  tuzo ya heshima kwa wachezaji wa zamani pamoja na tuzo ya mwanasaisa aliyesaidia katika maendeleo ya michezo Afrika. 
Madhumuni ya kuandaa tuzo hii ni kuongeza ushindani kwenye ligi ya Tanzania Bara, pamoja na timu za taifa jambo litakalofanya kila mchezaji kujituma zaidi kulingana na majukumu analiyonayo kwenye timu. 
Ni imani yetu kwamba hatua hii itaongeza uwajibikaji na utelekezaji wa majukumu kwa moro pia itaongeza moyo wa uzalendo kwa wachezaji wa kitanzania kwenye timu za taifa.

Comments