TFF YAOMBOLEZA KIFO CHA MJUMBE WAKE


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha mjumbe wake wa Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Shabani Semlangwa kilichotokea Julai 5 mwaka huu kutokana na maradhi.
ACP Semlangwa ambaye alizikwa juzi (Julai 6 mwaka huu) katika Kijiji cha Gumba, Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani alitoa mchango mkubwa akiwa mjumbe wa Kamati hiyo inayoongozwa na Kamishna wa Polisi (CP) mstaafu Alfred Tibaigana.

Msiba huo ni pigo kwa familia ya ACP Semlangwa, TFF na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango na mawazo aliyotoa kwa shirikisho akiwa mjumbe wa kamati hiyo.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu ACP Semlangwa, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki cha msiba huo mzito. Pia TFF itatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.

Mungu aiweke roho ya marehemu ACP Shabani Semlangwa mahali pema peponi. Amina

Comments