SIMBA YAWAKUMBUKA MAFISANGO,OKWI





KOCHA Mkuu wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic amesema ubovu wa kikosi chake unatokana na pengo la nyota wake wawili, mshambualiaji wa kimataifa wa Uganda Emmanuel Okwi na marehemu Patrick Mafisango. 
Hatua hiyo inafuatia Okwi kuwa katika majaribio nchini Australia na Mafisango ambaye alifariki dunia usikua wa kuamkia Mei 17 jijini Dar es Salaam kwa ajali mbaya ya gari.
 Milovan alisema itachukua muda kupata mbadala wa wachezaji hao hasa ikizingatiwa kuwa kikosi chake cha sasa kina wachezaji wengi wageni, hivyo kushindwa kucheza kitimu. 
Alisema uwepo wa Okwi na Mafisango katika kikosi cha msimu uliopita, kulichangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya timu hiyo ikiwemo kutwaa ubingwa wa ligi kuu bara, hivyo anachofanya kwa sasa ni kukijenga kikosi chake ili kiwe katika mfumo mmoja na kwa bahati nzuri  mwelekeo wake unaonekana sasa.




Comments