MAKINDA YA RWANDA 'U20' YAWASILI KUIVAA NGORONGORO HEROES


Timu ya Taifa ya Rwanda ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 inatarajia kuwasili Dar es Salaam leo mchana (Julai 13 mwaka huu) kwa ndege ya RwandAir kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki dhidi ya Ngorongoro Heroes. 
Rwanda yenye msafara wa watu 27 wakiwemo wachezaji 20 itafikia hoteli ya Sapphire. Mechi hizo zitachezwa Julai 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Chamazi na Julai 16 mwaka huu Uwanja wa Taifa. 
Ngorongoro Heroes tayari iko kambini chini ya Kocha Jakob Michelsen na msaidizi wake Adolf Rishard kujiwinda kwa mechi hizo ambazo ni sehemu ya maandalizi ya kuivaa Nigeria. 
Mechi dhidi ya Nigeria ambayo ni ya kwanza ya raundi ya pili kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Algeria itachezwa Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Comments