Mwakilishi wa Jimbo la Raha Leo, Salim Nassor,
akimkabidhi tuzo ya Msanii Bora Chipukizi wa mwaka, msanii Emma Score, wakati
wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki
wa Zanzibar wa mwaka 2012.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mama Zakhia Bilal, akiwa ni miongoni mwa wageni waalikwa
waliohudhuria hafla hiyo.
Mkurugenzi wa redio ya Briz Fm, bi. Mariam, akimkabidhi
Tuzo ya kuwa msanii bora wa Kike wa muziki wa Afro Pop, Msanii Baby J, wakati
wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki
wa Zanzibar wa mwaka 2012.
Kundi la Taarab la Zanzibar One Modern Taarab, wakitoa
burudani jukwaani wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Abdallah Mwinyi Mkuu,
akimkabidhi Tuzo mwanamuziki wa kundi la Taarab la Zanzibar One Modern Taarab,
Saada Nassor, baada ya kuibuka mshindo kwa kuwa Msanii bora wa Kike wa mwaka wa
muziki wa Taarab ya Kisasa, wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa
Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012.
:- Mbunge wa Jimbo la Uzini na Mkurugenzi wa redio ya Zenji
Fm, Mohamed Seif Khatib, akimkabidhi Tuzo msanii, Rukia Ramadhan, aliyeibuka
mshindi kwa kuwa mwimbaji bora wa mwaka wa Taarab Aslia.
Baadhi ya wageni na wadau wa sanaa, waliohudhuria hafla
hiyo.
13:- Picha ya pamoja baada ya zoezi la kukabidhi zawadi kwa
washindi wa tuzo hizo.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo
ya Heshima msanii mstaafu wa muziki wa Taarab, Mwanacha Hassan Kijole (65)
wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa
muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012, zilizodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi
ya Zantel.Hafla hiyo ilifanyika jana Julai 6, 2012 katika Ukumbi wa Hoteli ya
Bwawani mjini Zanzibar. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Uzini na Mkurugenzi wa
redio ya Zenji Fm, Mohamed Seif Khatib (kushoto) ni Mkurugenzi wa Biashara wa
Kampuni ya Zantel, Zanzibar, Mohamed Baucha.
picha zote na muhidin Sufian -OMR
Comments
Post a Comment