MAHAKIMU KAGAME CUP KUPIGWA MSASA KESHO


boniface Wambura-msemaji TFF
Mtihani wa utimamu wa mwili (fitness test) kwa waamuzi walioteuliwa kuchezesha michuano ya Kombe la Kagame inayoanza Jumamosi (Julai 14 mwaka huu) utafanyika kesho (Julai 12 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Waamuzi 15 walioteuliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuchezesha michuano hiyo. Waamuzi hao wanawasili leo jijini Dar es Salaam. 
Kwa upande wa waamuzi wa kati (centre referees) ni Anthony Ogwayo (Kenya), Dennis Batte (Uganda), Israel Mujuni (Tanzania Bara), Issa Kagabo (Rwanda), Thierry Nkurunziza (Burundi), Farah Aden Ali (Djibouti) na Waziri Sheha (Zanzibar). 
Waamuzi wasaidizi (assistant referees) ni Elias Kuloba (Kenya), Peter Sabatia (Kenya), Musa Balikoowa (Uganda), Hamis Changwalu (Tanzania Bara), Jesse Erasmo (Tanzania Bara), Simba Honore (Rwanda), Abdulahi Mahamoud (Djibouti) na Josephat Bulali (Zanzibar).

Comments