Na Ruhazi Ruhazi
NINAAMINI
nguvu iliyotumiwa na Mwenyekiti wa Chama cha soka la wanawake (TWFA) Madina
Kessy na viongozi wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kwa upande mwingine
kujaribu kuzima kashfa ya usagaji iliyoikumba timu ya soka ya wanawake ‘Twiga
Stars’ ingetumika kwa ajili ya maendeleo ya soka la wanawake, tungekuwa mbali.
Twiga
Stars timu inayookoteza wachezaji wa kuichezea baada ya TWFA na TFF kushindwa
kuendesha Ligi soka ya taifa ya wanawake, iling’olewa na Ethiopia katika mechi za mwisho za kusaka tiketi
ya fainali za Afrika zitakazofanyika Novemba, Mwaka huu Guinea ya Ikweta.
Timu
hiyo ilikosa tiketi hiyo kwa kufungwa mabao 2-1 ugenini Adis Ababa, Ethiopia na
viongozi wa timu hiyo akiwemo aliyekuwa Kocha Mkuu wake Charles Boniface Mkwasa
wakaja na utetezi kwamba kilichowaangusha ni hali ya hewa na hujuma
waliyofanyiwa na wapinzani wao.
Hata
hivyo, utetezi wao ulikuwa dhaifu kwani wakicheza mechi ya marudiano mbele ya
maelfu ya Watanzania kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam , waligungwa tena
bao 1-0,
hivyo safari ya Guinea
ya Ikweta, ikaishia hapo.
Baada ya
hapo, harakati za kumsaka mchawi zikaanza kwa kuibuliwa suala la wachezaji
wa timu
hiyo kukosa maadili ya kisoka, likiwemo suala la kusagana, hivyo kuathiri
ufanisi
wa timu
hiyo dimbani.
Hili
likawachoma na kuwaumiza mno viongozi wa TWFA akiwemo Madina na Meneja wa Twiga
Stars, Furaha Francis wakiamua kuitisha mkutano kwenye ofisi za TFF.
Lakini, ili
kupata utetezi wa haja juu ya jambo hilo ,
waliamua kumjumuisha mpaka aliyekuwa kocha wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa,
licha ya kwamba alishajiuzulu kuinoa timu hiyo kutokana na matokeo mabaya.
Nilistaajabu
kuona viongozi hao wakionekana kuguswa na kuhamanika kwa madai hayo ya kashfa
lakini sivyo wanavyoguswa na kukosekana kwa Ligi soka ya wanawake nchini.
Ni hapo
ambapo kila mdau wa soka atahisi na kuziamini hisia zake kwamba kinachowafanya
viongozi hawa kutikisika kwa kashfa ndogo kama hiyo ni kutokana na kuhisi kuwa
maslahi yao
yataharibika, lakini wakisahau kuwa kutosimama kidete kuhakikisha kuwa soka la
wanawake nchini linapiga hatua tayari ni dosari inayotishia ulaji wao.
Kibaya
ni kwamba sio Madina, Furaha wala Kocha aliyeeleza namna walivyofanya uchunguzi
wao ili kujiridhisha kuwa kashfa hizo hazipo kwa wachezaji wao, zaidi ya kusema
mwenye ushahidi ajitokeze na kuwathibitishia.
Nilitamani
kucheka kwa sababu sote twafahamu kuwa waandishi waliandika kile walichoelezwa
kwa hiyo ilikuwa juu yao
kufanyia uchunguzi kabla ya kutaka kujisafisha kwani masuala hayo hufanyika kwa
siri hivyo wao walipaswa kufanya uchunguzi wa siri pia, sio kutka tu
kujisafisha eti kwa hofu kuwa wazazi wataanza kuwazuia watoto wao wa kike
kujifunza na kucheza soka.
Ni wazi
kuwa, kashfa hizi za usagaji zisingeibuliwa kama Twiga Stars ingeishinda Ethiopia
na kutinga fainali za Afrika kwa wanawake.
Tangu tulipoanza kukutana na Ethiopia katika fainali za kuwania
kufuzu kwa mashindano mbali mbali ya soka kwa wanawake mwaka 2002, hatujawahi
kushindwa hata mchezo mmoja.
Nakumbuka
kuwa Ethiopia
waliwahi kuambulia sare ya mabao 2-2 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es
Salaam
(Uhuru)
mwaka huo wa 2002, lakini sisi tukasonga kwa sababu tuliwafunga mabao 3-2
nyumbani kwao.
Lakini,
katika kuonesha kuwa hakuna kinachofanywa kukuza soka la wanawake nchini,
safari hii Ethiopia
imetufunga katika michezo yote miwili.
Hata
hivyo, kiashirio cha kushuka kwa kiwango cha soka letu kilionekana pale
tulipokubali kuwa gunia la mazoezi la
timu za Zimbabwe na Afrika Kusini ‘Banyana Banyana’
ambazo zilitufunga idadi kubwa ya mabao kwwenye uwanja wa taifa tulipocheza
nazo mechi za kirafiki wakati tukijiandaa kucheza na Ethiopia .
Nakumbuka
siku akina Madina na wenzake wakihangaika kujisafisha na kashfa ya usagaji pale
TFF, nilimuuliza haoni haja ya kujiuzulu kwa kushindwa kulisaidia soka la
wanawake lipige hatua kiasi kwamba ameshindwa hata kuasisi michuano maalum
itakayohusisha Mikoa yote nchini kama
ameshindwa kuendesha Ligi soka ya wanawake, majibu yake yakawa “Siwezi
Kujiuzulu”.
Hata
hivyo, nilimtafakari jinsi Madina anavyotaka asafishwe kiasi cha kufikia hatua
ya kuomba kukutana na vyombo vya habari ili tu aondokane na kashfa hiyo ya
usagaji inayosemwa kila kona ya nchi hivi sasa ambayo inadaiwa kuwa chanzo cha
kuvuja kwa siri hiyo ni baadhi ya wachezaji wenyewe wa Twiga, ambao wamesema
kuwa wapo wenzao waliokubuhu kwa mchezo huo ndio maana viwango vyao vimeshuka.
Ni hapo
hoja ya umuhimu wa kuwepo kwa Ligi soka ya wanawake inapokuwa na mashiko,
lakini kwa bahati mbaya sana Madina na wenzake wa
TFF hawalioni hilo ,
zaidi ya kubaki wakijinasibu kwamba hupokea mgao maalum kutoka Shirikisho
la soka
la Kimataifa (FIFA) kwa maendeleo ya soka la wanawake.
Kwa
sababu kuwepo kwa Ligi kutapanua uwigo wa kocha wa Twiga Stars kuchagua
wachezaji bora na wasio na kashfa, tofauti na sasa ambapo vyovyote atakavyofanya.
Sijui
watu hawa watatuambia maendeleo hayo ya soka la wanawake yanayopigiwa upatu
hata na FIFA ni yepi zaidi ya kuwa na Ligi bora pamoja vituo vya kuibua na
kuendeleza soka la wanawake?.
Nadhani
hii kashfa inayowaliza kwa baadhi ya wachezaji wao kuhusishwa na masuala ya
usagaji ni ndogo kama timu itaendelea kufanya
vibaya, huenda tukajionea au kusikia kashfa nyingine nzito zaidi ya hizo na
ambazo pengine zikawaweka pabaya zaidi viongozi hao, TFF na mustakabali wa soka
la wanawake kwa ujumla.
Comments
Post a Comment