WAAMUZI KOZI YA FIFA KUPIMWA UFAHAMU WA ALAMA


Waamuzi 54 wanaoshiriki kozi ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) iliyoanza Juni 11 mwaka huu, kesho (Juni 14 mwaka huu) watahamia Uwanja wa Karume kwa ajili ya mazoezi ya alama (signals). Mazoezi hayo yatafanyika kuanzia saa 1-4 asubuhi. 
Kozi hiyo itakayomalizika kesho (Juni 14 mwaka huu) inaendeshwa na wakufunzi Carlos Henriques na Mark Mizengo kutoka FIFA wakisaidiwa na wakufunzi wengine wanne wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). 
Wakufunzi wa TFF ni Kapteni mstaafu Stanley Lugenge, Leslie Liunda, Soud Abdi na Riziki Majala. 
Waamuzi wanaoshiriki ni 14 wa Tanzania wenye beji za FIFA ambao ni Erasmo Jesse, Ferdinand Chacha, Hamis Changwalu, Hamis Maswa, Israel Mujuni, John Kanyenye, Josephat Bulali, Judith Gamba, Mwanahija Makame, Oden Mbaga, Ramadhan Ibada, Saada Tibabimale, Samuel Mpenzu na Sheha Waziri. 
Washiriki wengine ni 20 wa daraja la kwanza (class one), kati ya hao watano wanatoka Zanzibar. Lakini vilevile wapo waamuzi chipukizi (watoto) 20 ambao mwaka jana walitumika katika michuano ya Kombe la Uhai na Copa Coca-Cola.
 Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
 

Comments