AZAM FC KUANZA KUJINOA J'3

MABINGWA wa kombe la Mapinduzi Azam Fc jumatatu ya keshokutwa inatarajiwa kuanza kujinoa kwa ajili ya michuano ya kombe la Kagame itakayoanza kutimua vumbi jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi huu.
Msemaji wa msaidizi wa Azam Fc Jaffer Idd Maganga amesema kwamba wachezaji wote wanatakiwa kuripoti kamni siku hiyo tayari kuanza mazoezi yao.
Azam Fc inayonolewa na Muingereza Stewart Hall, pia ni wa shindi wa pili wa ligi kuu soka Tanzabnia Bara

Comments