KINACHOENDELEA KWENYE MSIBA WA KANUMBA THE GREAT

Kwa mujibu wa blogu ya Bongo Starz:
MVUA inanyesha, lakini mamia ya watu wamejazana mchana huu nje ya nyumba aliyokuwa anaishi marehemu Steven Charles Kanumba, aliyefariki usiku wa kuamkia leo.
Nyumba hiyo ipo eneo la Sinza, mkabala kabisa na hoteli maarufu ya Vatican. Pande zote mbili za barabara inayotokea Sinza Kijiweni kuelekea Tandale Uzuri watu wamejazana.
Misururu ya watu imeanzia kwenye hoteli ya Deluxe, Sinza na wengine ambao wameamua kujiweka kwenye baa zilizo jirani na eneo hilo ili mradi washiriki kwa namna yoyote.
Nyumba zilizo jirani na nyumba aliyokuwa akiishi The Great Kanumba watu wamepanda juu ya kuta kuchungulia ndani ya nyumba ya staa huyo, nini kinaendelea.
Yote haya yanaashiria ni kiasi gani Steven Kanumba alikuwa kipenzi cha wapenzi wa filamu nchini. Kipenzi cha Watanzania.
Vilio, manung’uniko, sura za majonzi na simanzi, vyote vimetawala eneo la tukio. Hakika ni majonzi makubwa- na hata baadhi ya wanaume wanashindwa kujizuia. Wanalia. “Kanumba, Kanumba, why Lulu?” alisikika dada mmoja akisema huku analia, karibu kabisa na geti la nyumba aliyokuwa akiishi marehemu.
Ndani ya nyumba hiyo, watu hawaingii tena. Kumejaa. Getini kuna ulinzi mkali na idadi ya watu waliojazana getini ni sawa ile misururu ya kuingia kwenye mechi kubwa Uwanja wa Taifa.
Maoni ya watu ni kwamba, eneo ambalo watu wamekusanyika kwa sasa ili kuomboleza msiba huo halitoshi na wanapendekeza msiba huo upewe hadhi ya kitaifa kwa kupelekwa kwenye maeneo ya wazi.

KIFO CHAKE:
Kanumba
Kanumba alifariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo na chanzo cha kifo chake inaelezwa ni kugombana na mpenzi wake, mwigizaji mwenzake, Lulu.
“Alikuwa anagombana na Lulu. Lulu akamsukuma Kanumba, akaangukia kichwa, ndio akafa, ilikuwa saa tisa usiku,” kilisema chanzo.
Habari zaidi zinasema, wivu ndio chanzo cha ugomvi wao.
Inaelezwa Lulu alikuwa anazungumza na simu na Kanumba akataka kujua anaongea na nani.
Lulu hakutaka kumpa simu Kanumba na ndipo wakaanza kuvutana na mwenzake akadondoka chini.
Inaelezwa alidondokea kisogo katika eneo gumu na ndipo hali ikawa mbaya kabla ya kifo chake.

MWILI WA KANUMBA:
Waombolezaji

Kwa sasa mwili wa mwigizaji huyo wa picha la Big Daddy upo katika vyumba vya kuhifadhia maiti, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.
Mwili huo ulichukuliwa mara tu baada ya tukio lililosababisha kifo chake.
Kanumba ambaye filamu yake ya mwisho kuingia sokoni ni Tambua Haki, inayoendelea kuuzwa hivi sasa, imeelezwa kwamba Lulu ndio chanzo cha kifo chake.
Ndugu wa Kanumba ambaye alikuwa akiishi naye Sinza, jijini Dar es Salaam na wakati mauti yanamkuta- na aliyekuwapo nyumbani amethibitisha hayo alipohojiwa na waandishi wa habari.
Ndugu huyo amekaririwa akisema Lulu ambaye jina lake halisi ni Elizabeth Michael, alikuja nyumbani kwa Kanumba na kumkuta yeye (ndugu) amekaa na marehemu usiku.
Ndugu huyo anasema aliwaachia faragha wawili hao wazungumze, lakini baada ya muda akasikia malumbano na yalipozidi wakahamia chumbani, ambako waliendelea kugombana.
Anasema baada ya muda, Lulu alitoka chumbani akipiga kelele huku akimuita yeye (ndugu).
Anasema alipotokea, Lulu akasema Kanumba ameanguka chumbani na povu linamtoka mdomoni.
Ndugu huyo anasema alipokwenda chumbani, kweli alikuta hali hiyo, akaenda kumuita daktari.
Anasema aliporejea na daktari, katika hali ya kushangaza, akakuta Lulu amekwishatoweka, ndipo wakachukua mwili wa marehemu na kuupeleka Muhimbili.
LULU YUKO WAPI?
Kimwana Lulu

Tayari Lulu amekwishakamatwa na Polisi na amehifadhiwa Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam.
Chanzo cha habari kinasema Lulu amechanganyikiwa na tangu ahakikishiwe kwamba Kanumba amefariki dunia, hajitambui.
Bado ni kizungumkuti juu ya hatima ya Lulu na kifo cha Kanumba na ni taarifa ya Polisi pekee itakayoondoa utata kuhusu tukio zima hilo.
Ingawa siri ya mapenzi yao inafichuka baada ya kifo cha mwenzake, lakini Lulu katika mahojiano mbalimbali ambayo amekuwa akifanyiwa amekuwa akikakana kuwepo uhusiano wa aina yoyote kati yake na marehemu Steve.

MSIBA, MAZISHI:
Ndani kwa Kanumba
Bado pamoja na mvua kunyesha, eneo dogo, lakini bado watu wanakusanyika Sinza.
Ndani ya nyumba waliobahatika kuingia kwa wingi ni wasanii mastaa haswa, na watu wa karibu, lakini wengine wamekwama nje.
Kulingana na umaarufu wa Kanumba katika jamii, familia ya marehemu italazimika kushirikiana na serikali kupitia vitengo husika kama BASATA katika kuratibu mazishi ya nyota huyo aliyekuwa na kipaji kikubwa cha uigizaji.
Ni moja kati ya mawili, Kanumba atasafirishwa Shinyanga au atazikwa hapa hapa Dar es Salaam. bongostaz inaendelea kufuatilia kwa karibu na itaendelea kukupasha kila kitakachojiri.

Comments

  1. inasikitisha sana juu ya kifo cha jamaa yetu huyu steven kanumba.

    ReplyDelete
  2. Nani asiemtambua ama kumsikia ndugu yetu Kanumba?
    Mungu amlaze pahala pema peponi. Tutakukumbuka sana.

    ReplyDelete
  3. rest in peace brother as you will always be honoured for the great things and contributions in to thr movie industry and to the community at all

    ReplyDelete
  4. uuhh! kifo jamani!

    ReplyDelete
  5. He was a Tanzania Icon,Mungu amlaze mahali pema peponi kipenzi chetu steve.

    ReplyDelete
  6. Inasikitisha sana kumpoteza kijana ambaye amelitangaza Taifa letu, Mungu atupe nguvu kustahimili msiba pia amlaze mahali pema peponi. AMENI

    ReplyDelete
  7. kila jambo na wakati,ushauri wangu tujue kwamba kifo hakizuiwi na kitu chochote,ila na kazi yetu kukaa vizuri na Mungu ili wakati ukifika tuondoke vizuri.

    ReplyDelete
  8. mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi amen

    ReplyDelete
  9. Mungu amlaze mahal pema pepon inauma sn tena sn

    ReplyDelete
  10. We lov him bt God was lovin him more rest in peace brodda.....we gonna remember you coz no one like you.......THE GREAT KANUMBA.....

    ReplyDelete
  11. pengo lake halitazibika haraka

    ReplyDelete
  12. how l wish hako kalulu kafungwe ili iwe fundisho kwa wengine wenye vihere kama yeye na waswhili wanasema ukiona mwenzako ananyolewa na wewe tia maji so thoz who they think they no better than god should becareful with god coz there an he does not like wat u guyz r doing so heads up live like other person an stop doing stupid thingz in order kupata umarufu ambao mwisho wa siku unaishia pabaya by the way pooooooole lulu but u nid to learn ur lesson babygirl an stop being jlo.....

    ReplyDelete
  13. To God be da glory.Eyes and ears have really witnessed your presence as well as ua prominence to people's mind across da country.U've truely gone out of people's will,consequently,leaving da majority with breathlessness and become unconscious cuz of ua departure.we won't see u anymore but ua sense of humor shall prevail for ever and ever.May ua soul,"Kanumba da great", rest in peace.for sure, u're a man of da people

    ReplyDelete
  14. Hv baada ya kufa kanumba ndo imekuwa neema kwa wengine au?au ndo wanafuata msemo unaosema kuwa kufa kufaana?maana 2meckia mengiyakiongelewa juu ya kifo cha THE GREAT,kwamba wa2 wanauza mali zake mara wenine wakijifanya wana mtoto wake,kwan toka alipokuwa hai mbona hapakuwa na m2 aliyejitokeza na kusema kuwa an mtoto ili aweze kuhudumiwa na mwenyewe THE GREAT.Jamani WATZD 2ache uswahili kwani ukizdi sana ni noma,alf haipendez.

    ReplyDelete

Post a Comment